Katibu Mkuu Wizara ya
Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbas ameongoza mapokezi ya wawekezaji zaidi
ya 150 kutoka Taifa la Marekani ambao wamewasili katika Kiwanja cha Ndege cha
Kimataifa cha Kilimanjaro (KIA) majira ya saa moja na nusu kwa ndege ya Shirika
la Oman.
Wawekezaji hao wanatarajia
kutembelea vivutio mbalimbali nchini ikiwemo Hifadhi bora Afrika kwa mara tano
mfulululizo Serengeti pamoja na kivutio bora Afrika kwa mwaka 2023 ‘Ngorongoro’
lengo likiwa ni kujionea fursa mbalimbali za uwekezaji zinazopatikana katika
vivutio hivyo ambapo wanatarajia kutumia zaidi ya siku 10 katika vivutio hivyo.
Aidha Dkt. Abbas,
aliongozana na viongozi mbalimbali wa Taasisi za Uhifadhi kutoka TANAPA na
Ngorongoro.
Na. Edmund Salaho- Kilimanjaro
0 Maoni