Dkt. Abbas aongoza mapokezi ya wawekezaji zaidi ya 150 kutoka Marekani

 

Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbas ameongoza mapokezi ya wawekezaji zaidi ya 150 kutoka Taifa la Marekani ambao wamewasili katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro (KIA) majira ya saa moja na nusu kwa ndege ya Shirika la Oman.

Wawekezaji hao wanatarajia kutembelea vivutio mbalimbali nchini ikiwemo Hifadhi bora Afrika kwa mara tano mfulululizo Serengeti pamoja na kivutio bora Afrika kwa mwaka 2023 ‘Ngorongoro’ lengo likiwa ni kujionea fursa mbalimbali za uwekezaji zinazopatikana katika vivutio hivyo ambapo wanatarajia kutumia zaidi ya siku 10 katika vivutio hivyo.

Aidha Dkt. Abbas, aliongozana na viongozi mbalimbali wa Taasisi za Uhifadhi kutoka TANAPA na Ngorongoro.

Na. Edmund Salaho- Kilimanjaro

Chapisha Maoni

0 Maoni