Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) imesaini mkataba wa
makubuliano ya awali kati yake na ujumbe kutoka Nchini China wenye lengo la
kutekeleza mradi wa kuboresha uendelezaji wa Jiopaki ya Ngorongoro– Lengai
Utekelezaji wa mradi huo unatarajiwa kuanza mwanzoni mwa
mwaka 2024 na utafanyika kwa kipindi cha miaka miwili kwa gharama ya shilingi bilioni
25 ambazo zitatolewa na Serikali ya China.
0 Maoni