Mkazi wa Kisiwa cha Maisome
wilayani Sengerema mkoani Mwanza, Maisala Ramadhani (25) ameangua kilio
mahakamani baada ya kuhukumiwa kwenda jela miaka 20 baada kukiri kosa la
kukutwa na dawa za kulenya aina ya Bhangi nyumbani kwake.
Hukumu hiyo ya kesi ya jinai
namba 121/2023, imetolewa jana Novemba Mosi, 2023 na Hakimu Mkazi wa Mahakama
ya wilaya ya Sengerema Evod Kisoka.
Awali, akisoma maelezo mbele
ya hakimu, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Morice Mtoi amesema mshitakiwa
alikamatwa Oktoba 9, 2023, na Mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai wa Wilaya ya
Sengerema, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Titho Mohe.
Mwendesha mashtaka huyo
amesema mshtakiwa alikamatwa na askari huyo katika kisiwa cha Maisome kambi ya
wavuvi ya Migongo akiwa na Bhangi kilogramu 10 kwenye nyumbani kwake
Wakili wa Serikali, Morice
Mtoi amesema mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo kinyume na Kifungu namba15A(1) (2)(c)
cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na dawa za kulevya Sura ya 95 toleo la mwaka
2019 kama ilivyofanyiwa mabadiliko na sheria ya mabadiliko ya sheria mbalimbali
namba 5 ya mwaka 2021.
Pamoja na maombi ya
mshtakiwa (Maisala) kuomba kupunguziwa adhabu, Mahakama imemhukumu kifungo
hicho cha miaka 20 ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo
kulingana na madhara yasababishwayo na madawa ya kulevya.
0 Maoni