Ukitaka kumiliki gari Singapore kwanza lipa sh milioni 266

 

Gharama ya cheti cha kumiliki gari la familia nchini Singapore imeongezeka na kufikia rekodi ya juu ya dola 106,619, sawa na shilingi 266,929,622 za Tanzania.

Serikali ya nchi hiyo ilianzisha mfumo wa malipo ya cheti cha umiliki gari kwa muda wa miaka 10 (COE) mnamo mwaka 1990 ikiwa ni sheria ya kukabiliana na msongamano wa magari.

Mtu anayetaka kumiliki gari nchini Singapore anapaswa kuwa na cheti hicho cha COE, ili apatiwe ridhaa ya kununua gari.

Vyeti hivyo huuzwa kwa mnada kila baada ya wiki mbili, huku Serikali ya Singapore ikidhibiti idadi ya vyeti vinavyouzwa.

Kwa kodi na ushuru wa forodha, mfumo huo umeifanya nchi ya Singapore kuwa nchi ghali mno duniani kwa mtu kununua gari.

CHANZO: BBC

Chapisha Maoni

0 Maoni