Serikali yaja na mpango wa kukomesha migogoro ya wakulima na wafugaji

 

Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imesema kampeni ya upandaji wa malisho ya mifugo na uchimbaji wa visima na malambo katika mashamba ya wakulima binafsi inalenga kutatua migogoro ya ardhi nchini.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Alexander Mnyeti amesema hayo wilayani Mvomero mkoani Morogoro wakati akihitimisha jukwaa la maandalizi ya kampeni hiyo ijulikanayo kama "Tutunzane Mvomero" na kusema migogoro mingi ya ardhi imekuwa ikitokana na kutokuwa na mpango wa matumizi bora ya ardhi katika vijiji na kwenye maeneo ambayo tayari mipango hiyo usimamizi wake unakuwa hafifu.

Kampeni hii ina kauli mbiu isemayo “Mfugaji mtunze mkulima na mkulima mtunze mfugaji ili kulinda mazingira yetu” inalenga kuwaelimisha kwanza kuanza kumiliki ardhi kwa ajili ya kuoata malisho ya mufugo yao na kuanza kufuga mifugo inayoendana na eneo la ardhi wanayomiliki ili kuondokana na migogoro ya ardhi ambayo imekuwa ikijitokeza mara kwa mara kutokana na wafugaji kuhamahama.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri huyo wa Mifugo na Uvuvi amewahimiza wafugaji kuendelea kumiliki maeneo kwa ajili ya ufugaji na kufuata sheria na taratibu zilizopo ili wasiingie kwenye migogoro ambayo inaweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Wizara ya Mifugo na Uvuvi imejipanga kuhakikisha haki inatendeka kwa kila mwananchi hivyo ikiwa kosa linakuwa kwa mfugaji au mkulima basi kila mmoja atachukuliwa hatua kulingana na sheria na taratibu zilizopo.

Chapisha Maoni

0 Maoni