Cristiano Ronaldo amefunga magoli mawili wakati Ureno
ikiichakaza Bosnia-Herzegovina magoli 5-0 katika mchezo wa kuwania kufuzu Euro
2024.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 38, aliifanya Ureno
kuongoza kwa mkwaju wa penati kabla ya baadae kufunga goli lake la kimataifa la
127, na kufanya matokeo kuwa 2-0.
Katika mchezo huo Ureno ambao walikuwa ugenini walifunga
magoli hayo matano kabla ya mapumziko kupitia kwa Bruno Fernandes, Joao Cancelo
na Joao Felix.
Kwa matokeo hayo Ureno ambayo ilishafuzu Euro 2024 tangu siku
ya Ijumaa, inabakia kileleni mwa kundi J ikiwa na ushindi wa asilimia 100.
0 Maoni