Rais wa Marekani Joe Biden atatembelea Israel Jumatano
kupatiwa taarifa ya mipango ya vita dhidi ya wapiganaji wa kundi la Hamas.
Marekani imesema Rais Biden ataelezwa namana Israel
itakavyofanya oparesheni katika namna ambayo itapunguza madhara kwa raia.
Wakati huo huo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony
Blinken, amesema Washington imefanikisha kuhakikishiwa na Israel kuruhusu kuingizwa
misaada ya kibinadamu Gaza.
Taarifa zaidi zinasema maelfu ya watu wa Gaza wamekusanyika kwenye
mpaka wa Rafah ili kuingia Misri wakati jitihada za Kidiplomasia zikiendelea
kufungua mpaka huo, kabla ya kuanza vita ya aridhini.
0 Maoni