Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema kuwa kila
mwanachama wa Hamas atauawa, kauli ambayo ameitoa baada ya mkutano wa kwanza wa
dharura wa serikali.
Akiwa pamoja na kiongozi wa kambi ya upinzani Benny Gantz,
Netanyahu amesema kuwa ni muda wa vita sasa.
Hata hivyo, Rais Joe Biden wa Marekani ameongea na Netanyahu
na kumueleza wazi Israel inapaswa kuzingatia sheria za vita.
Vifo vilivyotokea Israel vimefikia watu 1,200, huku nako
watu zaidi ya 1,100 wameuawa katika mashambulizi ya Israel huko Gaza.
0 Maoni