Aliyekuwa Makamu wa Rais wa Marekani Mike Pence, amejitoa
kwenye mbio za kinyang’anyiro cha urais wa Marekani 2024, akisema kwamba huu si
wakati wake.
Pence aliyekuwa Makamu wa Rais wakati wa utawala wa Rais
Donald Trump, ametangaza kujitoa kwenye kongamano la wanachama wa Republican
Wayahudi huko Las Vegas, Jumamosi mchana.
Pence anakuwa mgombea wa kwanza mwenye jina kubwa wa chama
cha Republican kusitisha kampeni zake katika mbio za urais ambazo kwa chama
hicho Donald Trump bado anaongoza.
Makamu huyo wa rais wa zamani wa Marekani, amekuwa hafanyi
vyema kwenye kura za maoni na pia amekuwa akishindwa kupata kura za wanachama wa
Republican.
0 Maoni