Nyerere atangaza rasmi vita na Idi Amin ukumbi wa Karimjee
'Sisi kama wanachama halali wa umoja huu tulitaka jambo moja
tu lifanyike na nilimjulisha Mwenyekiti wetu wa OAU Rais Jaffeir Nimeir wa
Sudan kuwa Amin amefanya jambo la makusudi na mimi naliita la makusudi kabisa
kwamba ameingia Tanzania ambayo ni taifa huru akachukua sehemu ya kipande cha
ardhi ya Tanzania akaikalia kimabavu, tukaijulisha OAU kwamba tunachotaka sisi
ni jambo dogo sana kwamba OAU itoe tamko la kumlaani tu Amini kuwa kitendo hiki
si cha kiungwana hata...hata kidogo. Sasa madhali OAU iliamua kukaa kimya leo
nimekuja kuwaambieni kuwa sasa tunaitangazia Dunia kuwa Tanzania tunayo kazi
moja tu kuwa ni kumpiga Amin; uwezo tunao, sababu tunayo na nia tunayo.
Tunaomba mataifa marafiki wasituambie kuhusu suluhu bali wajue kuwa tunayo kazi
hii na ikibidi waje watusaidie'
Dk. Julius Kambarage Nyerere Oktoba 1978 Karimjee Hall.
0 Maoni