Jeshi la Israel linapanga kuanza kufanya mashambulizi ya
aridhini, angani na baharini katika eneo la ukanda wa Gaza.
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amewaambia
wanajeshi kuwa mashambulizi ya aridhini yanatarajiwa kuanza, na kuongeza kuwa “hatua
inayofuata inakuja”.
Israel imewaonya Wapalestina milioni 1.1 wanaoishi kaskazini
mwa Gaza kuondoka kupitia kusini na maelfu wamekuwa wakikimbia vita kwa kutumia
magari.
Shirika la Afya Duniani (WHO) limelaani amri ya watu
kuondoka Gaza na kusema hali ya kulazimisha wagonjwa waliopo hospitalini
kuondoka ni sawa na hukumu ya kifo.
0 Maoni