Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk.
Hussein Ali Mwinyi leo amekagua miradi miwili akianzia mradi wa ujenzi wa
kiwanda cha kusarifu dagaa cha ZAFICO na amewaagiza Jeshi la Kujenga Uchumi-JKU
ambao ni mkandarasi kuwalipa fidia wananchi waliovunjiwa vibanda vyao.
Dk. Mwinyi amewapa JKU hadi tarehe 08 Desemba mwaka huu wawe
wamekamilisha ujenzi wa mradi huo atatembelea tena maendeleo ya ujenzi.
Aidha, Rais Dk. Mwinyi akizungumza na wananchi katika eneo
la mradi Wilaya Magharibi A Mkoa wa Mjini Magharibi, ameagiza walipwe fidia zao
na atafuatilia kuhakikisha wanalipwa stahiki zao haraka wakiwemo vibarua
waliolalamika kucheleweshewa malipo yao.
Baadae Dk. Mwinyi akatembelea mradi wa bandari kavu Maruhubi
Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi. Eneo hilo linatumika kuhifadhi na
kutoa makasha au makontena.
0 Maoni