Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Mpogolo amewataka
wafanyabiashara nchini kuchangamkia fursa kwa kurasimisha biashara zao Wakala
wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) ili kunufaika na biashara
wanazozifanya.
Mhe. Mpogolo ametoa wito huo jana, alipotembelea Maonesho ya
BRELA na wadau wake yanayofanyika katika uwanja wa Mlimani City Jijini Dar es
Salaam.
Mhe. Mpogolo amesema lengo la maonesho ya BRELA ni kuhamasisha
wadau kurasamisha biashara zao kwa wingi
hasa kipindi hiki ambacho BRELA imeandaa maonesho na kuzishirikisha taasisi mbalimbali za Umma na kutoa huduma
mahali pamoja.
Aidha, Mhe. Mpogolo amefafanua kuwa mfanyabiashara
anaporasimisha biashara yake hutambulika na taasisi za kifedha, humwezesha kupata zabuni mbalimbali pamoja na kuwa rasmi
kisheria.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Halima
Bulembo ameipongeza BRELA kwa kuandaa Maonesho yenye tija kwa wafanyabiashara
na kwa ukuaji wa uchumi nchi.
“Nimefurahishwa sana na huduma nzuri inayotolewa na BRELA,
hivyo basi wafanyabiashara ambao bado hawajarasimisha biashara zao ni vyema
wakafuata taratibu sahihi za kusajili,” amesema Mhe. Bulembo.
Maonesho haya ya siku tano (5) ya BRELA na Wadau wake yenye
Kauli Mbiu "Urasimishaji biashara katika Mapinduzi ya Nne ya Viwanda” yalifunguliwa Oktoba 24, 2023
na yatahitimishwa Oktoba 27, 2023 Sambamba na Mkutano wa BRELA na Wadau wake
utakaofanyika katika ukumbi wa Mlimani
City Jijini Dar es Salaam.
0 Maoni