Watoto wawili ambao ni mapacha wenye umri wa miaka 17 wakazi
wa Kijiji cha Bubale katika Kata ya Nkololo Wilayani Bariadi Mkoani Simiyu
wamefariki dunia baada ya kupewa dawa na mganga wa jadi kwa lengo la
kuwaongezea ukubwa wa matiti ili waweze kuolewa.
Mwenyekiti wa Kijiji cha Byuna ameeleza kuwa mganga huyo
anaitwa Masunga Tumolo na majirani wamekiri kuwa watoto hao walikuwa kwa mganga
huyo Kijiji cha Byuna ambako walikwenda kuoga dawa ya kuwaotesha matiti.
Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Byuna, Dkt. Deogratius
Mtaki amesema awali alipokea mwili wa Dotto na baadae akampokea Kulwa akiwa
mahututi baada ya muda mfupi naye akapoteza maisha.
Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Simon Simalenga ambaye alifika
katika eneo la tukio hilo amekemea kitendo hicho na kulitaka Jeshi la Polisi
kuwachukulia hatua wale wote waliohusika na tukio la mauaji ya mabinti hao.
0 Maoni