Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Mbarali, Bw. Missana
Kwangura amesema shughuli ya kupiga kura kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo hilo
imemalizika salama na kwamba kinachoendelea kwa sasa ni kazi ya kuhesabu kura
kwenye vituo vyote 490 vya kupigia kura na kuwasilisha matokeo ya vituo kwenye
kituo cha kujumuisha na kutangaza matokeo.
Bw. Kwangura amevitaka vyama vya siasa, wagombea na wapiga
kura kuwa wavumilivu wakati kazi ya kukusanya matokeo kutoka vituoni ikiendelea
na kwamba matokeo yatatangazwa mara baada ya kukamilika kwa kazi ya majumuisho
ya kura.
0 Maoni