Polisi wamfungulia mashtaka muuaji wa rapa Tupac Shakur

 

Polisi Marekani wamemfungulia mashtaka kiongozi wa genge la uhalifu, kwa mauaji ya rapa Tupac Shakur mwaka 1996, yaliyoacha maswali mengi kwa umma kwa muda mrefu.

Msanii huyo mashuhuri wa muziki wa hip-hop aliyezaliwa Jijini New York Marekani, alipigwa risasi nne na kufa akiwa kwenye gari barabarani huko Las Vegas.

Ijumaa, Mahakama ya Juu ya Nevada, imemfungulia kesi Duane "Keffe D" Davis, 60, akikabiliwa na shtaka la mauaji hatari ya kutumia silaha.

Polisi wamesema Keffe D, alipanga mauaji hayo ya Tupac baada ya binamu yake kugombana na Tupac Shakur kwenye Casino.

Duane "Keffe D" Davis alikamatwa nyumbani kwake Las Vegas mapema jana na atafikishwa mahakamani katika siku za hivi karibuni.

Picha iliyotolewa na Polisi Marekani ikimuonyesha kiongozi wa genge la uhalifu Duane "Keffe D" Davis, anayeshtakiwa kwa mauaji ya rapa Tupac Shakur 

Chapisha Maoni

0 Maoni