Zoleka Mandela, mjukuu wa rais wa kwanza aliyechaguliwa Kidemokrasia
Afrika Kusini, Nelson Mandela, amefariki dunia kwa ugonjwa wa saratani akiwa na
umri wa miaka 43.
Zoleka amefariki dunia jumatatu jioni akiwa amezungukwa na
marafiki pamoja na familia yake, Msemaji wa familia ya Mandela ameeleza.
Katika miaka ya hivi karibuni, Zoleka alifahamika kwa
kuelezea vyema umma matibabu ya saratani anayopatiwa. Pia aliweka wazi historia
yake ya kuwahi kuwa teja wa dawa za kulevya.
CHANZO: BBC
0 Maoni