Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Julius Mtatiro ametoa wito kwa
Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) kutoa elimu kwa
Wachimbaji Wadogo husasan ya vito Wilayani humo ili kuwajengea uwezo kwenye
uchimbaji, uchenjuaji na uchukuaji wa sampuli za madini.
Mtatiro ameyasema hayo wakati akipokea Kitabu kinachoonesha madini
yapatikanayo Tanzania kilichoandaliwa na GST kwa lengo la kuhamasisha uwekezaji
kwenye Sekta ya Madini hususan katika tafiti za kina.
Aidha, Mtatiro ameipongeza GST kwa kuandaa na kusambaza
Vitabu hivyo ambavyo vitasadia kutambua aina na maeneo gani madini hayo
yanapatikana.
0 Maoni