Raphael Varane amefunga goli dakika 14 kabla ya mpira
kumalizika na kuipa ushindi wa bahati Manchester United dhidi ya Wolves katika
mchezo wao wa kwanza wa Ligi Kuu ya Uingereza.
Kikosi cha kocha Erik ten Hag kilitengeneza nafasi za
kutafuta goli kwa shida hadi pale Bruno Frenandez alipompatia pande safi ndani
ya boksi Aaron Wan-Bissaka.
Beki huyo wa kulia wa United alitulia na kunyanyua mpira kwenye
eneo la goli ndipo Varane alipotumia urefu wake kuruka juu ya Nelson Semedo na
kufunga goli la kichwa.
0 Maoni