Kamishna wa Umeme na Nishati Mbadala wa Wizara ya Nishati,
Mhandisi Innocent Luoga amesema Tanzania inatarajia kupokea ujumbe kutoka
Serikali ya Malawi watakaofika nchini kwa ajili ya majadiliano kuhusu
ushirikiano wa nchi hizo katika Sekta ya Nishati.
Mhandsi Luoga amesema hayo kwa Niaba ya Katibu Mkuu wa
Wizara hiyo, Mhandisi Felchesmi Mramba, wakati wa kikao cha maandalizi ya
kupokea ujumbe huo kilichofanyika jijini Dar Es Salaam, Agosti 7, 2023 kwa
kushirikisha maafisa kutoka Wizara ya Nishati na Taasisi zilizochini yake,
Wizara ya Mambo Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Ofisi ya Mwanasheria
Mkuu wa Serikali, Wizara ya Maji na Wizara ya Fedha.
Ujumbe huo utapokelewa na mwenyeji wao Waziri wa Nishati,
January Makamba, unatarajiwa kuwasili nchini Agosti 9, 2023, utakaoshirikisha
Waziri wa Nishati wa nchi hiyo na Viongozi wengine waandamizi katika masuala ya
Nishati na Maji kutoka nchini humo.
0 Maoni