Sweden yaonyesha kiwango bora na kuitoa nje Japan

 

Nchi ya Sweden imeonyesha kiwango bora na kufanikiwa kutinga nusu fainali ya kombe la dunia wanawake kwa kuifunga Japan magoli 2-1.

Japan ilikuwa inaonekana kama inania ya kutwaa kombe hilo, baada ya kutinga hatua ya 16 bora kwa kuifunga timu ya Norway.

Katika mchezo wa leo Japan walifungwa goli la kwanza na Amanda Ilestedt na kisha kiungo wa Manchester City Filippa Angeldahl kuongeza goli la pili kwa mkwaju wa penati

Japan walipatiwa penati yenye utata lakini mkwaju uliopigwa na Riko Ueki dakika ya 76 uligonga mwamba, ndipo baadae Honoka Hayashi akaifungia Japan goli pekee dakika ya 87.

Chapisha Maoni

0 Maoni