Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein
Ali Mwinyi amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itaendeleza ushirikiano
uliopo na kujifunza zaidi kati ya Wizara pamoja na Taasisi zake za Serikali ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ameyasema hayo alipokutana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais,
Mipango na Uwekezaji Mhe.Prof Kitila Mkumbo aliyefika Ikulu Zanzibar na ujumbe
wake leo tarehe 05 Agosti, 2023.
Aidha, Rais Dk. Mwinyi amewapongeza na kuwashukuru ujumbe
huo kwa utayari wa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa mawazo
ya kimageuzi yanalolenga kujenga uchumi wa wananchi wa pande zote mbili katika
ushirikiano wa Taasisi zinazohusu Mamlaka ya Bandari, Ofisi ya Msajili Hazina,
Mamlaka za Uwekezaji pamoja na Tume ya Mipango ya Taifa.
Ujumbe ulioongozana na Waziri Prof.Kitila pamoja na Katibu
Mkuu Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Dk. Tausi Kida, Msajili wa Hazina
Nehemia Mchechu, Katibu wa Tume ya Mipango Lawrence Mafuru, Mkurugenzi Mkuu
EPZA Charles Itembe, Mkurugenzi Mkuu TIC Gilead Teri na Mkurugenzi wa
Miundombinu TPA Dk. Hussein Lufunyo.
🗓️05 Agosti, 2023
📍Ikulu, Zanzibar
0 Maoni