Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Exaud Kigahe,
ameitaka jamii kuwajenga watoto malezi yasiyo na hofu wakati wa wa hatua za
makuzi ili wawe raia wema na wenye kujiamini wanapokuwa wakubwa.
Kigahe ametoa rai hiyo alipotembelea Banda la Wizara ya
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum katika viwanja vya John
Mwakangale kwenye maonesho ya Nane Nane Kitaifa yanayoendelea mkoani hapa.
"Ni ukweli kwamba, jamii ikiwajenga watoto katika
kujiamini na kujisimamia katika wakati wa utoto wao utawawezesha kujiamini hata
wanapokuwa watu wazima" amesema Kigahe.
Kigahe amepongeza juhudi zinazochujuliwa na Wizara hususan
ni kukabiliana na vitendo vya ukatili na kusisitiza kwamba, jamii ikiwa na
ukatili hata shughuli za uzalishaji Mali haziwezi kutendeka.
Awali Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Wizara ya Maendeleo ya
Jamii, Jinsia Wanawake na Makundi Maaalum Regina Molel amemuelezea Naibu Waziri
huyo huduma mbalimbali zinazotolewa na Wizara hiyo ikiwepo huduma za msaada wa
kisaikolojia, uwezeshaji wanawake kiuchumi na usajili wa Mashirika Yasiyo ya
Kiserikali.
"Sisi kama Wizara tunashiriki maonesho haya kwa mara
pili mfululizo hivyo, tunajitahidi sana watu waelewe shughuli zetu ikiwepo usimamizi
wa Taasisi zetu mbili na vyuo Nane vya Maendeleo ya Jamii " amesema
Regina.
Mbali na Naibu Waziri kutembelea banda hilo la Wizara watu
wengine waliotembelea ni pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mjini Mhe. Beno
Malisa ambaye ameiomba Wizara kuendelea kutoa elimu ya kupinga ukatili kwa
watembeleaji wa maonesho hayo.
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi
Maalum ni moja ya Wizara inayoshiriki maonesho hayo ambayo yanafanyika Kitaifa
mkoani Mbeya.
Na WMJJWM Mbeya
0 Maoni