Simba waliovamia Kijiji na kuibua taharuki wauawa mkoani Njombe

 

Simba waliozua taharuki maeneo mbalimbali ya vijiji vya mikoa ya Njombe na Iringa wameuawa leo tarehe 7 Agosti 2023 kitongoji cha Lole Kijiji cha Makungu Wilaya vya Mufindi kwa ushirikiano wa askari wa Jeshi la Uhifadhi wa wanyama pori toka Kipengere

Mkuu wa Hifadhi ya Wanyama Pori Kipengere Mkoani Njombe Bw. Donasiani Makoye amesema simba hao walitoweka hifadhini mnamo tarehe 21 Julai 2023.

Na wao kama Jeshi la Uhifadhi waliendelea kuwafuatilia simba hao na leo hii tarehe 7 Agosti 2023 wamefanikiwa kuwauwa

Mhifadhi huyo amekiri kuwa Simba hao wamesababisha madhara makubwa kwa kushambulia na kuuwa ng'ombe 14 na nguruwe 5 hadi kuuawa kwao hii leo.

Aidha, Mhifadhi huyo amesema wao Jeshi la Uhifadhi wanaendelea kuchukua hatua zaidi ili kuwadhibiti simba hao ikiwa pamoja na kuwafungia mfumo wa mawasiliano wa utambuzi

Kwa upande wao wananchi wa Kata ya Makungu wamesema kwa muda mrefu wameshindwa kuendelea na majukumu yao kwa kuhofia simba hao wakiendelea kuongea na Mufindi Fm Radio wananchi hao wamesema wanawashukuru askari hao wa Hifadhi ya Kipengere kwa kuwauwa simba hao na kutoa rai kwa serikali na mamlaka husika kuja na namna sahihi ya kuwadhibiti simba hao wasitoke kwenye hifadhini.

Na. Anton Kuyava- Mufindi Fm Radio

Chapisha Maoni

0 Maoni