Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema ujio wa msanii nyota maarufu wa filamu nchini China, Jin Dong utaifungulia milango zaidi Zanzibar kwa soko la watalii kutoka China na kuitangaza kimataifa.
Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo leo Ikulu, Zanzibar
alipokutana na msanii huyo ambaye yupo Zanzibar kwa ajili ya kutengeneza
filamu.
Aidha, Rais Dk. Mwinyi alimueleza msanii huyo kuwa Zanzibar
ina vivutio vingi vya utalii ikiwemo utalii wa fukwe za bahari zenye mchanga
mweupe zinazovutia wengi duniani, utalii wa utamaduni, utalii wa Mji Mkongwe, utalii
wa michezo, utalii wa visiwa pamoja na wa Mikutano.
Vilevile, Rais Dk. Mwinyi amemtembeza katika miongoni mwa
vivutio msanii huyo ikiwemo kisiwa cha Mnemba, maeneo ya Mizingani, Forodhani
pamoja na Mji Mkongwe.
Msanii Jin Dong ni nyota mkubwa China mwenye ushawishi na
wafuasi katika mitandao ya kijamii zaidi ya Milioni 15 pia na kazi zake nyingi
za filamu alizoigiza nchini humo.
🗓️10 Agosti, 2023
📍Zanzibar.
0 Maoni