Lionel Messi amefuta hofu ya kuumia na kufunga goli lake la
tisa katika michezo sita akiwa na Inter Miami, wakiifunga Philadelphia Union na
kutinga fainali ya kombe la ligi.
Raia huyo wa Argentina mshindi wa kombe la dunia aliifungia
Miami goli la pili katika ushindi wa magoli 4-1, siku moja tu baada ya kuumia
kwenye enka mazoezini.
Josef Martinez, Jordi Alba na David Ruiz nao waliifungia
magoli Miami, huku naye Alejandro Bedoya akiwafungia wenyeji goli pekee.
0 Maoni