Rais wa FIFA aahidi kuja Tanzania uzinduzi wa Super League

 

Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) Gianni Infantino amesema kuwa anaielewa vizuri Tanzania na kuahidi kuwa atakuwapo kwenye uzinduzi wa michuano ya Africa Super League itakayofanyika nchini, Jijini Dar es Salaam.

Hayo yameelezwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Klabu ya Simba, Salim Tryagain, ambaye amekutana na Infantino pamoja na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu FIFA Omella Desiree Bella.

Tryagain ameeleza hayo kupitia kwenye ukurasa wa akaunti yake ya mtandao wa twitter na kuongeza kuwa amejadiliana na viongozi hao wa FIFA kuhusu michuano ya Africa Super Legue, akiwa huko Park Hyatt, Jijini Sydney nchini Australia.

Tryagain yupo Sydney kushiriki kozi ya Diploma katika uongozi na klabu inayotolewa na FIFA (Diploma in Club Management), pia kujifunza shughuli za mpira na jinsi mashindano makubwa yanavyoandaliwa.

Timu ya Simba ndio timu pekee ya Tanzania itakayoshiriki mashindano hayo, timu nyingine ni Petro de Luanda- Angola, TP Mazembe- DR Congo, Al Ahly- Egypt, Horoya- Guinea, Wydad Casablanca- Morocco, Esperance- Tunisia na Mamelodi Sundowns- Afrika Kusini.

Chapisha Maoni

0 Maoni