Mbrazili Fabinho naye atimkia Saudi Arabia

 

Kiungo Mbrazili Fabinho amekamilisha uhamisho wa kuhamia klabu ya Saudi Arabia ya Al-Ittihad kutoka Liverpool.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29, hakuwepo kwenye kambi ya Liverpool waliyokaa Ujerumani, baada ya timu hiyo ya Saudi kutoa ofa ya paundi milioni 40.

Fabinho pia aliachwa na Liverpool katika safari yao ya Singapore kwa lengo la kumuwezesha kukamilisha mpango wake wa kuhamia Al-Ittihad.

Chapisha Maoni

0 Maoni