Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk.
Hussein Ali Mwinyi amesema malengo ya Serikali katika sekta ya afya ni
kuhakikisha wananchi wa Zanzibar wanapata huduma bora za afya.
Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo leo Agosti 14, 2023 wakati akifungua
kituo cha afya Bumbwini Makoba, Wilaya ya Kaskazini B Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Aidha, Rais Dk. Mwinyi alieleza katika hatua za awali
zinazofanywa na Serikali katika sekta ya afya ni kuhakikisha wananchi wa
Zanzibar wanapata huduma bora kufikia malengo ya kuimarisha miundombinu kwa
kujenga hospitali za Wilaya kila Wilaya, hospitali za Mkoa kila Mkoa na
hospitali ya Binguni itakayokuwa kubwa zaidi na kutoa huduma za uchunguzi
Zanzibar.
Pia hatua nyengine Serikali imeamua kushirikiana na sekta
binafsi zitoe huduma katika hospitali za serikali zinazohusisha uchunguzi wa
maradhi mbalimbali.
0 Maoni