Beki wa kati wa Simba Hennock Inonga leo atafanyiwa vipimo kubaini ukubwa wa jeraha alilopata jana wakati timu ya Simba ikiibua na ushindi wa mkwaju ya penati 4-2 dhidi ya Singida Faountain Gate.
Hennock alishindwa kumaliza mchezo wa nusu fainali Ngao ya
Jamii dhidi ya Singida Fauntain Gate jana baada ya kuumia bega.
Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally
amesema Inonga atafanyiwa uchunguzi wa kitabibu leo, Wanasimba watapewa taarifa
kuhusu hali yake
"Ni kweli Inonga aliumia jana, alitoka uwanjani akiwa
na maumivu makali sana ya bega. Alipatiwa huduma ya kwanza, sasa anaendelea
vizuri. Kesho (leo) madaktari watamfanyia uchunguzi kubaini ukubwa wa jeraha
ili kuona kama atahitaji matibabu zaidi au la," alisema Ally.
Simba ilitinga fainali ya Ngao ya Jamii kwa ushindi wa
mkikwaju ya penati 4-2 baada ya matokeo ya suluhu ya bila kufungana dhidi ya
Singida Fauntain Gate.
0 Maoni