Waziri Mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu, amefanyiwa
upasuaji wa dharura na kuwekewa kifaa cha kurekebisha mapigo ya moyo
(pacemaker) baada ya kupelekwa hospitali usiku wa Jumamosi.
Madaktari wa hospitali ya Shena Medical Centre wamesema
upasuaji huo umefanyika vizuri, na Netanyahu hayupo katika hali ya kuhatarisha
maisha yake.
Kuugua na kulazwa hospitali Bw. Netanyahu, kumekuja wakati
ambao bunge la nchi hiyo linaelekea kupiga kura muhimu ya mabadiliko ya mfumo
wa Mahakama.
Maandamano yanayopinga mabadiliko hayo yamesambaa Israeli,
huku wafanyakazi wengi wakiapa kugoma iwapo muswada huo utapitishwa na bunge.
0 Maoni