Wanajeshi wa Niger watangaza kumpindua rais Bazoum

 

Wanajeshi wa nchi ya Afrika ya Magharibi ya Niger wametangaza kufanya mapinduzi kupitia televisheni ya taifa.

Wanajeshi hao wamesema wameifuta Katiba, na kusitisha shughuli zote za taasisi pamoja na kufunga mipaka yote ya nchi hiyo.

Rais wa Niger Mohamed Bazoum, anashikiliwa na vikosi maalum vya ulinzi wa rais tangu mapema siku ya Jumatano.

Marekani imemuahidi kumpatia ushirikiano usio na shaka, kwa njia ya simu iliyopigwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Antony Blinken.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) António Guterres naye amesema ameongea na rais Bazoum na kumuhakikishia kuwa Un inamuunga mkono.

Rais Bazoum wa Niger ni mdau muhimu wa mataifa ya magharibi katika mapambano dhidi ya makundi ya wanamgambo wa kiislamu Afrika ya Magharibi.

Chapisha Maoni

0 Maoni