JKCI yapanga kuanza kutibu tatizo la nguvu za kiume

 

Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), inatarajia kuanza kutoa huduma ya kuzibua mishipa ya uume ikiwa ni hatua ya kukabiliana na upungufu wa nguvu za kiume kwa wanaume wenye tatizo hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Dar es Salaam, Mkurugenzi wa JKCI Dk. Peter Kisenge, amesema huduma hiyo inatarajiwa kuanza mwezi Oktoba mwaka huu.

Dk. Kisenge amesema tatizo hilo ni kubwa japo hakuna utafiti walioufanya, lakini wapo wanaume wenye tatizo hilo wanaofika kwenye taasisi ya JKCI.

“Tutakwenda kuanzisha huduma mpya ambapo tutashirikiana na wenzetu wa India, kwani tatizo la nguvu za kiume linazidi kuongezeka kwa mishipa ya uume kuziba,” amesema Dk. Kisenge.

Dk. Kisenge amesema “tatizo lipo na pengine hilo ni siri ya wagonjwa hatuwezi kuweka wazi ila huduma itaanza mwaka huu”.

Chapisha Maoni

0 Maoni