Tume
imependekeza mamlaka ya kipolisi ya kukamata na kuweka mtuhumiwa kizuizini
waliyonayo Wakurugenzi wa Halmashauri na Maofisa Watendaji wa Kata yaondolewe
na jukumu hilo liachwe kwa Jeshi la Polisi.
Mapendekezo
hayo na mengineyo yametolewa na Tume ya kuboresha mfumo na taasisi za haki
jinai nchini, wakati ikiwasilisha rasmi mapendekezo yake kwa Serikali.
Mapendekezo
hayo yamewasilishwa mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan leo Ikulu, Dar es Salaam
na Mwenyekiti Tume ya Haki Jinai, Jaji Mstaafu, Mohamed Chande.
Jaji
Mkuu Mstaafu Chande amesema tume imebaini kuwa mamlaka ya kukamata imetolewa
kwa taasisi nyingi na kwa watu wengi ambao wamevishwa mamlaka ya kipolisi.
0 Maoni