Watu
wapatao 22 wamekufa, kufuatia mafuriko makubwa Korea Kusini, wakati mvua kubwa
zikiendelea kunyesha katika mikoa ya kati.
Katika
siku ya tatu ya mvua kubwa, kumetokea maporomoko ya ardhi, na kusababisha bwawa
kubwa katika mkoa wa Chungcheong kufurika maji.
Mvua
hizo kubwa zimepelekea barabara kufunikwa na maji, magari kusombwa na maji, na
kutatiza usafiri wa reli.
Watu
wengine 14, wameripotiwa kutoweka na maelfu wamelazimika kuhama makazi yao,
maofisa wa nchi hiyo wamesema.
0 Maoni