Hali
ya joto kali Marekani, imetabiriwa kuongezeka mwishoni mwa juma hili, huku
tahadhari ikitolewa eneo la kusini magharibi mwa taifa hilo.
Hadi
kufikia Ijumaa, joto hilo liliwaathiri Wamarekani milioni 113, huko Florida,
Texas, California, hadi katika jimbo la kaskazini-magharibi la Washington.
Matumizi
ya viyoyozi katika jimbo la Texas, yaliongezeka na kufikia kiwango cha juu
katika jimbo hilo, na kuweka rekodi ya matumizi ya umeme.
Watu
wapatao milioni 27 nchini Marekani wametabiriwa watalazimika kukabiliana na
hali ya joto inayofikia nyuzi joto 43, katika siku zijazo.
0 Maoni