Tume ya Jinsi ya Kuboresha Taasisi za Haki Jinai nchini Tanzania imependekeza Jeshi la Magereza kufanyiwa mabadiliko ya kimuundo ili lifanye kazi zake kwa ufanisi.
Hayo
yamesemwa na Jaji Mkuu Mstaafu Mohamed Chande, wakati akiwawasilisha Ripoti ya Tume
ya Jinsi ya Kuboresha Taasisi za Haki Jinai, mbele ya Rais Samia Suluhu Hassan.
Jaji
Mkuu Mstaafu Chande amesema wamepokea taarifa za kuwapo kwa matumizi makubwa ya
nguvu katika Jeshi la Magereza na kushauri jeshi hilo libadilishwe liwe sehemu
ya kurekebisha tabia.
“Marekebisho
hayo ya kimuundo yanapaswa kuwafanyia mafunzo askari magereza pamoja na
magereza kuwa na shughuli za uzalishaji mali ili wafungwa wapate kujifunza
kazi,” amesema Jaji Mstaafu Chande.
Ameeleza
kwamba wamekutana na mfungwa mmoja ambaye yupo Dodoma kwa sasa ni fundi mzuri
wa nguo na anawashonea nguo hadi viongozi, ambaye alijifunza gerezani kwa
mfungwa mwenzake wa kutoka DRC.
Aidha,
tume hiyo imependekeza magereza kuachana na matumizi ya kuni ambayo hutumika kuwapikia
chakula cha wafungwa zaidi ya 31,000 nchini na kuchangia kuharibu mazingira.
“Tume
inapendekeza magereza sasa kuacha kutumia kuni, na badala yake watumie nishati
mbadala kama vile gesi, umeme na nishati nyingene rafiki kwa mazingira,”
amesema Jaji Mstaafu Chande.
0 Maoni