Rukhsa madaktari kufanya kliniki binafsi hospitali za umma

 

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu, ameruhusu madaktari wa hospitali za umma kufanya kliniki binafsi baada ya muda wa kazi kumalizika katika hospitali za Serekali nchini.

Mhe. Ummy ametangaza uamuzi huo mkoani Simiyu wakati akizungumza na watumishi wa hospitali ya rufaa ya Simiyu katika ziara yake aliyoifanya mkoani humo.

“Tusiweke urasimu daktari huyu baada ya saa kumi mruhusu afanyekazi zake za private (binafsi), wagonjwa wake wa private waje hapa atawaona mtakubaliana percentage (asilimia ya malipo),” alisema Waziri Ummy na kuongeza, “Hospitali ya Ocean Road nilifanya hivyo na MOI wewe mwenyewe unajua vizuri, madaktari wa Dar es Salaam wanahangaika kweli kijiwe hiki kijiwe kile, vijiwe hadi 120, daktari na muuguzi wanachoka sana”.

Mh. Ummy ameeleza kwamba kuna mgonjwa ambaye anataka aje kumuona daktari wakati hamna fujo, akute chumba kizuri kinamakochi, kuna maji, kuna chai, kuna kahawa, kuna soda na daktari atamuita muuguzi na kuchukua vipimo vyote hapo hapo.

Chapisha Maoni

0 Maoni