Mwanasoka Riyad Mahrez amekamilisha uhamisho kutoka Manchester City kwenda Ligi ya Saudi Pro katika timu ya Al-Ahli, kwa kitita cha paundi milioni 30
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32, anamuda wa miaka
miwili uliobakia kwenye mkataba wake, anaingia kwenye orodha ya nyota wakubwa
waliojiunga na ligi hiyo ya SPL.
Manchester City ililipa paundi milioni 60, kumnunua winga
huyo raia wa Algeria 2018, na aliifungia magoli 15 katika michezo 47, City ikitwaa
makombe matatu katika msimu uliomalizika.
0 Maoni