BASATA, TCRA yaufungia wimbo wa Ney Wa Mitego

 

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), limevitaka vyombo vya habari nchini kutopiga wimbo wa "Amkeni" uliotolewa hivi karibuni na msanii wa BongoFleva, Emmanuel Elibariki Kingu, maarufu kama Ney Wa Mitego.

Kwa mujibu wa taarifa, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imepokea barua ya Kaimu Katibu Mkuu wa BASATA, John Daffa kwenda TCRA, inayoagiza wimbo huo kutokupigwa kwenye mitandao ya kijamii na kwenye vyombo vya habari nchini.

Kwa mujibu wa BASATA, maudhui ya wimbo huo yana mwelekeo wa kutaka wananchi wasiwe na imani na Serikali, kuchochea wananchi kuwa na mapokeo hasi juu ya utekelezaji wa mipango ya Serikali yao kwa ujumla.

Barua hiyo ya Baraza la Sanaa Tanzania, pia imeongeza kuwa wimbo huo wa "Amkeni" ni wimbo wa uchochezi baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wananchi wake.

Chapisha Maoni

0 Maoni