Kiongozi wa Azimio Raila Odinga anaumwa na kwa sasa ameagizwa na daktari wake kupata mapumziko.
Raila hajaonekana tangu kuanza kwa maandamano ya kupinga kupanda kwa gharama za maisha pamoja na sheria mpya ya fedha ya 2023.
Akiongea kwa simu na gazeti la Nation Raila amesema ameanza
kupata nafuu, na muda sio mrefu atarejea kwenye majukumu yake, baada ya kupona
mafua makali.
Kuliibuka wasiwasi kuhusu alipo Raila Odinga jumatano, baada
ya kushindwa kuonekana katika maandamano ya kulalamikia hali ngumu ya maisha.
0 Maoni