Ulinzi umeimarishwa nchini Kenya kuelekea siku ya pili ya
maandamano yaliyopangwa kufanyika kwa siku tatu yaliyoitishwa na chama cha
Azimio.
Maandamano hayo yaliyoanza jana yameshuhudia kuwapo kwa
ulinzi mkali wa polisi waliowekwa kwenye maeneo hatarishi kwa usalama nchini
humo.
Wilaya ya Kati ya Kibiashara imezingirwa na makundi ya
polisi waliowekwa kuwadhibiti waandamanaji wasiingie kati kati ya Jiji la
Nairobi.
Wapinzani wameitisha maandamano hayo kushinikiza kupunguzwa
kwa gharama za maisha na kubadilishwa kwa Sheria ya Fedha ya 2023.
0 Maoni