Polisi nchini Kenya wamewatimua ndugu na marafiki wa mbunge
wa Embakasi Mashariki Babu Owino, waliovamia kituo cha polisi cha Wang'uru huko
Kirinyaga kushinikiza aachiwe.
Familia yake inasema mbunge huyo anashikiliwa kwenye kituo
hicho cha polisi, tangu akamatwe hapo jana.
Mbunge Owino alikamatwa jana asubuhi baada ya kutua na ndege
kwenye uwanja wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta, siku ya kwanza ya maandamano ya
Azimio.
0 Maoni