Nyumba ya mke wa aliyekuwa rais wa kwanza wa taifa la Kenya Hayati
Jomo Kenyatta, Mama Ngina Kenyatta iliyopo Muthaiga inalindwa na walinzi wa
kampuni binafsi baada ya serikali kumuondolea walinzi.
Kwa mujibu wa taarifa zilizoripotiwa na gazeti la Nation,
walinzi wa Mama Ngina waliondolewa jumanne usiku, baada ya ofisi za GSU na
Polisi wa Utawala kuwaagiza kuondoka na kuripoti kwenye kituo cha polisi.
Kuondolewa kwa walinzi hao, kumekuja baada ya Rais William
Ruto kudai kwenye mkutano wake huko Naivasha kuwa aliyekuwa Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, anawafadhili wapinzani kufanya maandamano ya kuipinga Serikali.
Mama Ngina, mama wa Uhuru Kenyatta alikuwa anapatiwa ulinzi
wa askari polisi 30 kulinda nyumba yake hiyo yote, kabla ya kupunguziwa na
kubakia polisi wanane mwaka 2022, na sasa ameondolewa polisi wote.
0 Maoni