Mtendaji Mkuu wa timu ya Simba SC Imani Kajula amesema
kwamba jezi tano za timu hiyo zitakazo zinduliwa juu ya kilele cha Mlima
Kilimanjaro zitakuwa na majina ya viongozi wa juu watano Serikali mgongoni.
Kajula ameyasema hayo na kutaja majina ya viongozi hao kuwa
ni ya Rais wa Jamhuri ya Muungano Dk. Samia Suluhu Hassan pamoja na Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ally Mwinyi.
Viongozi wengine ambao majina yao yamo kwenye jezi
hizo ni Makamu wa Rais Dk. Philip Mpango, Waziri Mkuu, Majaliwa Kassim Majaliwa,
Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson na Rais wa Heshima Mohamed Dewji Mo.
0 Maoni