Mkurugenzi Mkuu Bodi ya Utalii Tanzania Bw. Damasi Mfugale
amekutana na kufanya mazungumzo na Mh. Balozi wa Uingereza Nchini Tanzania Bw.
David Concar, katika kuendeleza programu ya kutembelea Balozi mbalimbali ili
kuimarisha mahusiano mazuri yaliyopo kati ya Tanzania na masoko ya kimkakati ya
utalii pamoja na masoko yanayoibuka,
Katika kikao hicho Bw. Mfugale na Balozi Concar wamejadili
fursa mbalimbali za ushirikiano kati ya Bodi ya Utalii na Ubalozi wa Uingereza
katika kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea Tanzania kutoka Uingereza
sambamba na kuvutia wawekezaji katika Sekta ya Utalii hususan kwenye maeneo ya
kimkakati ikiwemo Kusini mwa Tanzania.
0 Maoni