Zaidi ya watu 40 wamekufa huko Algeria, Italia na Ugiriki
wakati moto wa nyika wa Mediterranean ukielekea kuteketeza vijiji na hoteli za
mapumziko, huku maelfu wakihamishwa.
Ugiriki inajiandaa kufanya zoezi la kuwaondoa watu zaidi kwa
kutumia ndege kutoka Rhodes, wakati moto huo wa nyika ukishika kasi kueleka
visiwa Corfu na Evia.
Joto lililopo kwa sasa linaonekana pia kutokushuka chini na
badala yake linatarajiwa kupanda hadi kufikia nyuzi joto 44, katika maeneo ya
Ugiriki.
Moto huo wa nyika pia umewalazimisha maelfu ya watu kukimbia
makazi yao kwenye miji ya Sicily na Puglia.
Upepo mkali pamoja na mimea mikavu imechangia kuwapa wakati
mgumu zimamoto kuuzima moto huo na kukata maeneo ili moto usisambae.
0 Maoni