Lionel Messi atikisa nyavu mara mbili na kusaidia goli moja
katika mchezo wake wa mwanzo akiwa na Inter Miami katika ushindi wa magoli 4-0
dhidi ya Atlanta United.
Nyota huyo raia wa Argentina mwenye umri wa miaka 36,
alifunga magoli hayo mawili ndani ya dakika 22 za mwanzo na kumtengea goli Robert
Taylor katika kipindi cha pili.
Baada ya kufunga goli lake la pili, Messi alishangilia kwa
kumnyooshea kidole mmiliki wa Inter Miami mchezaji wa zamani wa Manchester
United na timu ya taifa ya Uingereza David Beckham.
0 Maoni