Manchester United, imekubali mpango kuinasa saini ya
mshambuliaji wa kimataifa wa Denmark Rasmus Hojlund kutoka Atalanta ya ligi ya
Sirrie A.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20, atahamia Old Traford kwa
dau la paundi milioni 64, pamoja na uwezekano wa kuongezewa tena paundi milioni
8.
Hojlund alijiunga na Atalanta Agosti 2022 na kufunga magoli 10
katika michezo 34 katika msimu uliomalizika.
Mkataba wake akiwa na United utakuwa wa miaka mitano, ukiwa
na uchaguzi wa kuongezewa utakapomalizika.
0 Maoni