Bondia Terence Crawford amemdunda Errol Spence Jr na kuwa
mshindi wa kwanza wa mikanda minne asiyepingika katika ubingwa wa welterweight.
Bingwa huyo wa WBO mwenye umri wa miaka, 35, alimtwanga
ngumi zilizomuangusha chini Spence mara tatu kabla ya refa kuamua kuingilia kati
na kumaliza pambano raundi ya tisa.
Kwa ushindi huo umemfanya Crawford kuwa binadamu wa kwanza asiyepingika
kwa kutwaa ubingwa wa mikanda ya mizani miwili tofauti.
0 Maoni